Home Makala Inonga Fiti Simba sc

Inonga Fiti Simba sc

by Dennis Msotwa
0 comments

Mashabiki wa klabu ya Simba sc sasa hawana budi kufurahi kufuatia kupona kwa beki wao mahiri Henock Inonga Baka ambaye alikua majeruhi baada ya kuumia katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Coastal Union na kulazimika kuwa nje kwa takribani majuma mawili.

Beki huyo ameonekana yuko fiti katika kambi ya timu ya Taifa lake la Congo Drc ambapo ameonekana akishiriki mazoezi kujiandaa na michezo miwili ya kirafiki dhidi ya New Zealand siku ya Oktoba 13 na ule dhidi ya Angola Oktoba 18.

Beki huyo aliumiza mapema katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Coastal Union baada ya kuchezewa rafu na mshambuliaji Hija Ugando ambapo alilazimika kukimbizwa hospitali na kushonwa jeraha hilo katika ugoko wake baada ya kuchanika na kulazimika kukaa nje kwa wiki mbili.

banner

Simba sc ililazimika kuwatumia Che Fondoh Malone na Kennedy Juma katika michezo miwili dhidi ya Tanzania Prisons na Singida Fountain Gate ambayo yote miwili walipata ushindi uliwafanya wajikite kileleni mwa msimamo wa ligi kuu nchini.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited