Home Makala Jeuri Kwishaa,Tshishimbi

Jeuri Kwishaa,Tshishimbi

by Sports Leo
0 comments

Baada ya Yanga kumpa siku 14, Papy Tshishimbi za kuamua hatma yake, jembe jipya kutoka Kagera Sugar, Zawadi Peter Mauya amesaini mkataba wa miaka miwili ili kuitumikia timu hiyo msimu ujao.
Mauya amesaini mkataba huo mbele ya mkurugenzi wa uwekezaji wa kampuni ya GSM inayoidhamini Yanga, Injinia Hersi Said, huku Kaimu Katibu wa Yanga, Wakili Simon Patrick akishuhudia.
Usajili wa kiungo huyo ni maandalizi kwa Yanga kujiandaa kuanza maisha mapya bila ya Tshishimbi ambaye kwa muda mrefu wamekuwa wakivutana katika suala la kusaini mkataba mpya.
Huu unakuwa usajili wa kwanza kwa Yanga kuelekea msimu ujao ambapo viongozi pamoja na wadhamini Kampuni ya GSM, wametamba kukisuka upya kikosi chao.

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited