Home Makala Kagere Kuikosa Yanga Novemba 7

Kagere Kuikosa Yanga Novemba 7

by Sports Leo
0 comments

Straika wa Simba Sc ,Meddie Kagere yuko hatarini kuikosa mechi ya watani wa jadi dhidi ya Yanga Sc kutokana na majeraha yanayomsumbua yatakayomfanya kukaa nje ya uwanja kwa takribani wiki tatu ili apone kabisa.

Ikumbukwe kuwa mechi ya watani ilitakiwa kuchezwa leo,Octoba 18 lakini bodi ya ligi kuu Tanzania(TPLB) ikasogeza mbele na hivyo itafanyiika Novemba 7,2020 uwanja wa Mkapa.

Uongozi wa Simba Sc kupitia kwa Ofisa Habari,Haji Manara amesema kuwa,Kagere ameongezeka kwenye listi ya ya majeruhi kikosini  kwao ambapo atakuwa nje kwa wiki tatu chini ya uangalizi maalum mpaka pale hali yake itakapotengemaa na kurejea uwanjani.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited