Home Soka Kagoma,Hamza Kuwakosa Kmc

Kagoma,Hamza Kuwakosa Kmc

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa klabu ya Simba Sc Fadlu Davis amesema kuwa mastaa Yusuph Kagoma na Abdulrazak Hamza wanatarajiwa kuukosa mchezo wa kesho wa ligi kuu ya Nbc nchini dhidi ya Klabu ya Kmc kutokana na kuwa na majeraha.

Fadlu amesema hayo mapema hii leo ikiwa ni katika mkutano na waandishi wa habari kama ilivyo utaratibu wa bodi ya ligi ambapo kila timu huzungumza waandishi siku moja kabla ya mchezo.

Mchezo huo utakaofanyika katika uwanja wa Kmc Complex uliopo Mwenge jijini Dar es Salaam ambapo Fadlu Davis amesema kuwa atawakosa mastaa hao kutokana na kuwa katika matibabu ya majeraha yao.

banner

“Kagoma na Valentino Mashaka bado wanakosekana ila Abdurazak Hamza ameanza mazoezi na wenzake japo hayupo tayari, pia hayupo kwenye mipango ya mchezo wa kesho dhidi ya KMC FC. Amesema Kocha Fadlu Davids.

Pia mshambuliajiwaklabuhiyoStephen Mukwala amesema kuwa wao kama wachezaji wanacheza kwa kujitoa kupambania nembo ya klabu hiyo.

“Tunacheza kwa kujitolea kwasababu ya nembo ya Simba SC halafu jina langu litakumbukwa baadae ila kwanza unajituma kwa ajili ya nembo ya Simba ndio maana sisi wachezaji hatukati tamaa hadi mwisho”. Alisema staa huyo aliyefunga bao la ushindi katika mchezo uliopita dhidi ya Mashujaa Fc .
Simba sc endapo itashinda mchezo huo itafikisha alama 25 na kuipiku Yanga sc ambayo ipo kileleni mwa msimamo wa ligi kuu ya Nbc nchini ikiwa na alama 24.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited