Home Makala Kamwe,Priva Wakiwasha Yanga sc

Kamwe,Priva Wakiwasha Yanga sc

by Sports Leo
0 comments

Waandishi wa habari Ally Kamwe na Priva Shayo wameanza cheche siku chache baada ya kutambulishwa kama watendaji wapya wa klabu ya Yanga sc katika nafasi za Afisa Habari na msimamizi wa maudhui wa klabu hiyo ambapo kwa nyakati tofauti tofauti wameonyesha jinsi gani mashabiki wa klabu hiyo walivyopakua applikesheni ya klabu hiyo pamoja na kutembelea website mpya.

Priva ambaye amejiunga na Yanga sc akitokea kituo cha redio cha Clouds Fm alipokua kama mchambuzi wa habari za michezo na amekwenda Yanga sc ambapo atakua msimamizi wa maudhui ya mitandaoni huku Ally Kamwe yeye ameenda klabuni hapo kama Afisa Habari akitokea Azam Tv alipokua mchambuzi wa masuala ya soka.

Yanga sc wameajiri watendaji wapya na kutambulisha pamoja na Afisa Mtendaji mkuu wa klabu hiyo Andre Mtine aliyechukua nafasi ya Senzo Mazingiza huku Kamwe akichukua nafasi ya Hassan Bumbuli na nafasi ya Priva ikiwa ni nafasi mpya klabuni hapo.

banner

Kamwe mapema hivi leo alikua katika mahojiano na kituo cha redio cha Wasafi ambapo alizungumza mambo mbalimbali kuhusu klabu hiyo hasa mchezo unafuata dhidi ya Al Hilal utakaofanyika siku jumamosi oktoba 8.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited