Beki wa klabu ya Simba Shomari Kapombe amekanusha taarifa zilizosambaa zikidai ametonesha majeraha yake wakati akifanya mazoezi na kikosi cha timu ya taifa kinachojiandaa na michuano ya Afrika (Afcon),Beki huyo mwenye uwezo wa kucheza kwa ufasaha nafasi zote za ulinzi na ile ya kiungo amekanusha taarifa hizo kupitia mitandao ya kijamii.
Katika taarifa iliyotolewa na akaunti ya mchezaji huyo kupitia mtandaa wa instagram ameonyesha kusikitishwa kwake na taarifa hizo huku akisisitiza kuwa yupo salama na hajajiunga na timu ya taifa kwa sababu ana programu maalumu aliyoachiwa na kocha wa viungo wa simba kwa ajili ya kurejesha utimamamu wa mwili.Taarifa aliyoitoa Kapombe ilisomeka kama ifuatavyo.