Home Makala Kayoko Akabidhiwa Derby

Kayoko Akabidhiwa Derby

by Sports Leo
0 comments

Mwamuzi wa Kimataifa wa Tanzania ,Ramadhan Kayoko Ndiye atakayechezesha Derby ya Kariakoo kati ya Yanga na Simba ambayo inatarajia kufanyika Jumapili ya wiki hii kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa Oktoba 23.

Kayoko amekua na uzoefu wa kuchezesha michezo hiyo akiwa ameshazesha mara kadhaa pasi kuzua malalamiko makubwa tofauti na wenzake mabao mara kadhaa wameshindwa kuhimili presha ya mchezo huo.

Refa huyo atasaidiwa na Ramadhani Mkono kutoka Tanga na Janeth Balama kutoka Iringa huku Mwamuzi wa akiba akiwa ni Elly Sasii kutoka Dar es salaam ambapo waamuzi hao kwa pamoja ndio watakaoamua hatma ya wababe hao wa ligi kuu nchini nani akae kileleni baada ya dakika tisini za mchezo huo ambao Yanga sc ndio watakua wenyeji.

banner

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited