Taarifa zinasema Uongozi wa Klabu ya Simba upo kwenye mazungumzo ya kutaka kumrejesha kiungo mshambuliaji Shiza Kichuya katika kikosi cha Wekundu hao kwa ajili ya msimu ujao wa ligi 2022/23.
Tayari mazungumzo ya kumrejesha Kichuya mpaka sasa yamefikia pazuri mabapo atasaini mkataba wa miaka miwili baada ya kuwa huru akiwa amemaliza mkataba wake katika klabu ya Namungo Fc yenye makao yake mkoani Mtwara ambapo alijunga akitokea klabu ya Pharco Fc ya nchini Misri.
Kichuya amekua na msimu mzuri katika klabu ya Namungo Fc msimu huu akiwa amechangia upatikanaji wa mabao nane akifunga matano na kusaidia upatikanaji wa mabao matatu katika ligi kuu msimu huu.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Simba sc awali iliwahi kumsajili Kichuya akitokea Mtibwa Sugar ambapo baada ya kucheza kwa misimu kadhaa klabuni hapo alikwenda nchini Misri katika klabu ya Pharco Fc ambayo ilimpeleka katika klabu ya Enppi alikocheza kwa mkopo kisha akarejea Simba sc na baadae kujiunga Namungo Fc.