Home Makala Kisa Mashabiki ,Yanga Yatozwa Faini

Kisa Mashabiki ,Yanga Yatozwa Faini

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Young Africans Sc imetozwa faini ya laki tano (500,000) kwa kosa la mashabiki wa timu yake kuonyesha vitendo vya utovu wa nidhamu kwa kuwapiga na kuwachania jezi mashabiki wanaohisiwa ni wa timu ya Simba Sc waliokuwa wamevaa jezi za simba kwenye mchezo uliochezwa Septemba,27 kati ya Mtibwa Sugar na Yanga Sc kwenye uwanja wa Jamuhuri jijini Morogoro.Adhabu hii imetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 45:1 ya ligi kuu kuhusu udhibiti wa klabu.

Mashabiki wawili wa yanga sc wanaofahamika kwa majina maarufu kama Osama na Jesca wamefungiwa kuingia uwanjani kwa kipindi cha miezi 12 kwa kosa la tukio la kushiriki kuwapiga na kuwachania jezi mashabiki waliokuwa wamevaa jezi za Simba Sc wakihisiwa kuwa ni wa timu hiyo iliyochezwa Septemba 27,2020 uwanja wa Jamuhuri mkoani Morogoro.

Katika kufanikisha maamuzi hayo picha za mashabiki hao zitabandikwa magazeti yote ya viwanja vinavyotumika kwa michezo ya ligi.

banner

Adhabu hii imetolewa kwa uzingativu wa kanuni ya 45:2 ya ligi kuu bara kuhusu udhibiti wa klabu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited