Home Makala Kisa Wasudan,Namungo Wajichia Zanzibar

Kisa Wasudan,Namungo Wajichia Zanzibar

by Sports Leo
0 comments

Namungo FC baada ya kumaliza mechi yake ya ligi dhidi ya Azam FC sasa inaelekeza nguvu zake kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika ambapo inajiandaa kucheza na El Hilal Obeid ya Sudan.

Namungo imeenda Zanzibar kujiandaa na mchezo huo ikiwa ni mapendekezo ya kocha Hemed Morocco ambaye anahitaji mechi mbili au tatu za kirafiki.

“Baada ya mechi yetu ya ligi tumegeukia mechi ya Kombe la Shirikisho ambapo tutacheza Disemba 23, 2020 dhidi ya El Hilal Obeid ya Sudan, tutacheza kwenye uwanja uleule wa Azam Complex Chamazi”-Hassan Zidadu, Mwenyekiti Namungo FC.

banner

“Mwalimu amependekeza timu ipate mechi mbili au tatu za kirafiki, tumeangalia ratiba za timu za hapa tumegundua hakuna nafasi kwa timu za ligi kuu wala ligi daraja la kwanza kwa hiyo tumeamua timu iende Zanzibar kwa sababu kuna viwanja vizuri na timu nyingi za kuchezanazo mechi za kirafiki.”

Credit:Shaffihdauda

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited