Home Makala Kumekucha Bunge Marathon

Kumekucha Bunge Marathon

by Sports Leo
0 comments

Waandaaji wa mbio za Bunge Marathon wamesema wameandaa mpango maalumu wa kukuza mchezo wa riadha kupitia mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika hivi karibuni April 12 2025 jijini Dodoma.

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari Mwenyekiti wa michezo wa Bunge Mh.Festo Sanga alisema kuwa fedha zitakazopatikana mwaka huu zitatumika kujenga shule ya wavulana ya Bunge katika eneo la Kikumbi jijini Dodoma.

banner

“Bunge la Tanzania limeshajenga Shule ya Sekondari ya Wasichana katika eneo la Kikombo, jijini Dodoma na sasa hivi tunashirikiana na watanzania kupitia Mbio hizi kujuenga Shule ya Sekondari ya Wavulana jijini Dodoma. Hivyo nawaomba watanzania mjitopkeze kwa wingi kushiriki katika mbio hizi alisema Mh.Sanga ambaye ni mbunge wa Makete.

“Mchango wa mbio za marathon utasaidia sekta ya elimu utaongozwa na Waheshimiwa Wabunge huku ikiambatana na dhamira ya Rais, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kukuza michezo na elimu, mbio hizi pia zinatoa fursa kwa Wabunge kuimarisha uhusiano wao na Watanzania sambamba na kuendeleza utimamu wa mwili na kuishi kiafya.” Amesema Mh.Sanga

Akizungumzia kuhusu zawadi kwa washindi Mheshimiwa Sanga amesema kwenye nusu marathon yaani kilometa 21, mshindi wa kwanza atajinyakulia Milioni 5, mshindi wa pili atapata Milioni 3 na mshindi wa tatu akiambulia Milioni 1.5.

Kwa upande wa kilomita 10, mshindi wa kwanza atazawadiwa shilingi milioni 2, mshindi wa pili Shilingi 1.5, na mshindi wa tatu atajinyakulia shilingi milioni moja huku. Katika kilomita 5 mshindi wa kwanza atapata shilingi 1.5, nafasi ya pili akipata milioni moja na mshindi wa tatu atapata shilingi laki tano.

Mbio hizo zitafanyika katika umbali wa kilomita kuanzia 5,10 na 21 huku kujiandikisha ikiwa ni shilingi za kitanzania elfu arobaini ambapo fedha hizo zitakazopatikana zitatumika kujenga shule ya Wavulana ya Bunge jijini Dodoma eneo la Kikombo.

Mbio za Bunge marathon zitafanyika Aprili 12 , 2025 zikiwa na matarajio ya kuvunja rekodi ya kuwa na washiriki zaidi ya 5,000kutoka ndani na nje ya nchi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited