Home Makala Mabingwa Fainali FA Wapokelewa Dar Leo

Mabingwa Fainali FA Wapokelewa Dar Leo

by Dennis Msotwa
0 comments

Kikosi cha Simba kimewasili leo jijini kikitokea Sumbawanga ambapo kilikuwa na mchezo wa fainali dhidi ya Namungo FC ambao walipigwa mabao 2-1 katika Uwanja wa Nelson Mandela.

Wanamsimbazi hao wamerejea na taji la kombe la shirikisho mjini ili  kuendeleza shangwe la ubingwa walioutwaa Sumbawanga kwani mashabiki ni ngao yao kubwa na wamekuwa bega kwa bega hivyo inabidi wafurahi kwa pamoja.

Wachezaji wa Simba wamepanda kwenye basi rasmi lililoandaliwa wakiwa na mataji mawili la Ligi Kuu Bara pamoja na Shirikisho wakiwa Kwenye msafara kuelekea Msimbazi.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited