Home Makala Makocha Azam Waongezewa Mikataba

Makocha Azam Waongezewa Mikataba

by Dennis Msotwa
0 comments

Azam Fc imewaongeza muda wa mikataba makocha wake katika benchi la ufundi  kwa ajili ya kuendelea kuwa ndani ya kikosi hicho kwa msimu wa 2020/21.

Makocha hao ni kocha mkuu, Aristica Cioaba, kocha msaidizi, Bahati Vivier na kocha wa viungo, Costel Birsan, ambapo kila mmoja ameongeza mkataba wa mwaka mmoja.

Azam Fc waliwatambulisha wachezaji wake wapya pamoja na benchi la ufundi siku ya Jumapili ambalo lilianza kazi kwa kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Namungo Fc na kuibuka na mabao 2-1 katika uwanja wao wa Azam Complex uliopo Chamazi.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited