Hatimaye golikipa namba moja wa Simba sc na Timu ya Taifa ya Tanzania Aishi Manula amefanyiwa upasuaji goti salama ili kutibu majeraha yake yaliyokua yakimsumbua na kusababisha kukosa michezo kadhaa ya ligi kuu na ile ya kimataifa.
Kipa huyo aliibukia katika klabu ya Azam Fc kisha akijiunga na Simba sc amefanyiwa upasuaji huo nchini Afrika ya kusini ambapo sasa atapewa mapumziko ya siku chache kisha atarejea nchini kuendelea na matibabu akisubiri kupona kabisa.
Manula amekua msaada mkubwa kwa klabu yake ya Simba sc na Taifa kwa ujumla huku akiwa ni moja ya makipa bora wa ligi kuu akichukua tuzo hiyo mara kadhaa.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Simba sc ilitoa taarifa kuwa ina mpango wa kumpeleka katika matibabu kipa huyo ili apone kabisa kwa ajili ya kuitumikia klabu hiyo katika msimu ujao wa ligi kuu nchini.