Home Makala Manyika Atua Singida FG

Manyika Atua Singida FG

by Sports Leo
0 comments

Aliyewahi kuwa mlinda mlango wa zamani wa timu ya taifa ya Tanzania Peter Manyika ametangazwa kuwa kocha mpya wa magolikipa wa klabu ya Singida Big Stars (Singida Fountain gates) yenye makazi yake mkoani Singida

Kipa huyo tayari ameanza kazi klabuni hapo na alikuwa sehemu ya benchi la ufundi la klabu hiyo kwenye mchezo dhidi ya Simba ambao walipoteza kwa mabao 2-1 siku ya Jumamosi jioni.

Mpaka sasa bado haijafahamika kocha amesaini mkataba wa muda gani lakini tayari amejiunga na miamba hiyo ya soka mkoani humo ili kuwasaidia makipa Benno Kakolanya na wenzake kuhakikisha wanakua na viwango imara.

banner

Manyika ni kipa wa zamani wa Yanga sc ambapo pia alikua akijihusisha na kazi ya kuwanoa makipa wachanga kutokana na uzoefu wake katika ngazi ya klabu na timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars).

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited