Home Makala Mastaa Yanga sc Warejea Mazoezini

Mastaa Yanga sc Warejea Mazoezini

by Sports Leo
0 comments

Mastaa wa klabu ya Yanga waliokua majeruhi Khalid Aucho, Pacome Zouzoua, Clatous Chama, Kennedy Musonda leo hii wamerejea mazoezini baada ya kupona majeraha yao.

Mbali na mastaa hao pia Yao Kouassi aliyekua na majeraha ya muda mrefu nae amerejea mazoezini licha ya kuwa hajaanza program za kufanya mazoezi na wenzake ndani ya uwanja.

banner

Daktari wa klabu hiyo Moses Etutu amesema kuwa mastaa hao wamerejea baada ya kupona majeraha kabisa ambapo Pacome Zouzoua,Cletous Chama na Kennedy Musonda wapo tayari kuanza kutumika kama kocha akiwahitaji huku Yao Kouassi akiendelea na mazoezi ya kutafuta utimamu wa mwili.

“Kutokana na mchezo ujao kuwa zaidi ya siku saba mbele wachezaji hao wapo tayari kutumika isipokuwa Yao Kouassi ambaye tunaendelea na matibabu ya kumpatia utimamu wa mwili ili awe sawa kama wenzake”,Alisema Daktari huyo.

Yanga sc katika msimamo wa ligi kuu ya Nbc nchini wana alama 70 wakiwa kileleni huku wakisaliwa na michezo mitatu pekee.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited