Home Makala Mayele,Diarra Watwaa Tuzo

Mayele,Diarra Watwaa Tuzo

by Sports Leo
0 comments

Wachezaji Fiston Mayele na Djigui Diarra wamefanikiwa kupata tuzo katika michuano ya kombe shirikisho iliyomalizika siku ya Jumamosi kutokana na kuonyesha viwango vizuri katika michuano hiyo.

Mayele amefanikiwa kuibuka kuwa mfungaji bora wa michuano hiyo akifunga mabao saba akiwazidi mastaa kama Ranga Chivahiro wa Marumo Gallants huku pia Djigui Diarra akiibuka kuwa mchezaji bora wa mchezo wa fainali ambao Yanga sc walishinda kwa 1-0 japo wamekosa ubingwa kwa sheria ya bao la ugenini.

Diarra amefanikiwa kuibuka kuwa Man of the match katika mchezo huo akifanya uokozi wa mashuti kadhaa huku pia akidaka penati iliyowarudisha Yanga sc mchezoni Yanga sc ambao walikua wanahitaji goli moja zaidi ili kupata ubingwa.

banner

Kipa huyo amekua gumzo nchini na Afrika mashariki kutokana na kiwango chake alichokionyesha katika michuano hiyo huku aina yake ya mpira ukiwemo uwezo wake wa kucheza kwa miguu imemfanya kuwa mchezaji wa ndani wa kumi na mbili hivyo kuipa faida Yanga sc katika michezo mingi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited