Home Makala Messi Atambulishwa Marekani

Messi Atambulishwa Marekani

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Inter Miami inayoshiriki ligi kuu ya soka Marekani (MLS) usiku wa kuamkia leo Jumatatu wamewatambulisha rasmi nyota wa Argentina Lionel Messi mbele ya washabiki zaidi ya 19,000 kwenye uwanja wao wa nyumbani DRV PNK Stadium.

Messi amejiunga na Inter Miami katika majira haya ya kiangazi baada ya mkataba wake na PSG kumalizika huku pia mchezaji mwenzake wa zamani wa Barcelona Sergio Busquets nae ametambulishwa kwenye timu hiyo ambapo amepewa jezi namba 5.

Messi aliamua kuondoka nchini Ufaransa katika klabu ya Paris St.German ambapo alijiunga akitokea klabu iliyomkuza ya Fc Barcelona licha ya kuwa na tetesi za kujiunga na timu za Uarabuni lakini mwishoni alijiunga na InterMiami inayoshiriki ligi kuu ya Major League Soccer ambayo hufupishwa kama Mls.

banner

Katika utambulisho pia matajiri wanaomiliki klabu hiyo walikuwapo wakiongozwa na David Beckham ambaye ana hisa klabuni hapo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited