Nyota wa zamani wa Yanga Saimon Msuva amesaini mkataba wa miaka mitatu kuitumikia klabu ya Benfica ya Ureno akitokea klabu ya Diffaa El-Jadid ya nchini Morroco.
Meneja wa nyota huyo Jonas Tiboroha amethibitisha kuwa licha ya kusainiwa na Benfica atapelekwa kwa mkopo Panathinaikos ya Ugiriki kwa miezi 6 hivyo Msuva atajiunga rasmi na Benfica mwezi Julai
Msuva alitua Difaa El Jadid akitokea Yanga aliyoitumikia kwa mafanikio makubwa miaka mitatu iliyopita.
Msuva atakuwa mchezaji wa pili kutoka Tanzania kusajiliwa na timu kubwa barani Ulaya akiungana na Mbwana Samatta anayekipiga KRC Genk