Home Makala Msuva Atua Ulaya Kibabe

Msuva Atua Ulaya Kibabe

by Sports Leo
0 comments

Nyota wa zamani wa Yanga Saimon Msuva amesaini mkataba wa miaka mitatu kuitumikia klabu ya Benfica ya Ureno akitokea klabu ya Diffaa El-Jadid ya nchini Morroco.

Meneja wa nyota huyo Jonas Tiboroha amethibitisha kuwa licha ya kusainiwa na Benfica atapelekwa kwa mkopo Panathinaikos ya Ugiriki kwa miezi 6 hivyo Msuva atajiunga rasmi na Benfica mwezi Julai

Msuva alitua Difaa El Jadid akitokea Yanga aliyoitumikia kwa mafanikio makubwa miaka mitatu iliyopita.

Msuva atakuwa mchezaji wa pili kutoka Tanzania kusajiliwa na timu kubwa barani Ulaya akiungana na Mbwana Samatta anayekipiga KRC Genk

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited