Home Makala Mudathir,Aggrey Wahitajika Simba sc

Mudathir,Aggrey Wahitajika Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Wachezaji Mudathir Yahaya na Aggrey Morris waliosimamishwa na klabu ya Azam Fc wapo mbioni kujiunga na klabu ya Simba sc iliyoonesha nia ya kuwasaini wote wawili pindi mazungumzo yatakapokamilika.

Wachezaji hao wameichezea Azam Fc na timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa stars) kwa mafanikio makubwa kwa nyakati tofautitofauti huku pia wakiwa na mchango mkubwa klabuni Chamazi yalipo makao makuu ya Azam Fc.

Kusimamishwa kwa muda usiojulikana inatajwa kuwa ni sababu ya wachezaji hao kuhitaji kuondoka klabuni hapo pamoja na kutuhumiwa kuwa watovu wa nidhamu na uongozi wa klabu hiyo.

banner

Simba sc inatajwa kuhitaji saini ya kiungo mmoja mzawa mwenye uwezo wa kushambulia na kuzuia kwa pamoja huku pia ikihitaji beki mbadala wa Serge Pascal Wawa ambaye amekalia kuti kavu pamoja na wachezaji kadhaa wa kimataifa akiwemo winga mshambuliaji Moses Phiri pamoja pia ikimhitaji Cletous Chama arejee baada ya kuonyesha nia ya kurudi huku pia ikitajwa Emmanuel Okwi naye akihitaji kurudi klabuni hapo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited