Home Makala Nabi Afungiwa Mechi 3

Nabi Afungiwa Mechi 3

by Sports Leo
0 comments

Kocha mkuu wa klabu ya Yanga sc Nasreddine Mohamed Nabi amkumbana na adhabu ya kukosa michezo mitatu na faini ya kiasi cha shilingi laki tano baada ya kuwashambulia kwa maneno waamuzi wakati wa mchezo baina ya klabu yake na Ihefu uliomalizika kwa Yanga sc kupoteza kwa 2-1 na kumaliza mwendo wa kucheza michezo 49 bila kufungwa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Bodi ya ligi kwa vyombo vya habari adhabu ya kocha huyo ni kwa mujibu wa kanuni ya 42:2(2.1) kuhusu udhibiti wa makocha.

Nabi kufuatia adhabu hiyo anatarajiwa kukosa michezo mitatu ijayo ya klabu yake ambayo itavaana na Prisons siku ya Jumapili huku ataukosa mchezo dhidi ya Namungo Fc utakofanyika mjini Ruangwa na ule wa kombe la shirikisho dhidi ya Kurugenzi Fc.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited