Home Makala Nabi Kupewa Heshima Maalum

Nabi Kupewa Heshima Maalum

by Sports Leo
0 comments

Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amesema katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya KMC ambao utapigwa jioni ya leo siku ya Jumatano katika uwanja wa Benjamin Mkapa, kutafanyika tukio maalum katika dakika ya 43 ya mchezo ili kumpa heshima kocha wao Nasreddine Nabi.
Tukio hilo ni kumpongeza Kocha Mkuu wa Yanga Nasreddine Nabi na benchi lake la ufundi kwa kuiongoza Yanga kucheza mechi 43 mfululizo za ligi pasipo kupoteza ambapo Itakapofika dakika ya 43, mashabiki watasimama na kupiga makofi kwa dakika moja ni ishara ya pongezi kwa benchi la ufundi kutokana na kuweka rekodi hiyo ya kibabe.
Nabi mpaka sasa hajapoteza mchezo wowote wa ligi kuu tangu apoteze kwa 1-0 dhidi ya Azam Fc katika mchezo wa ligi kuu uliofanyika mwishoni mwa msimu 2020 kwa bao la shuti la mbali kutoka kwa mshambuliaji Prince Dube hali ambayo imewapa jeuri mashabiki wa klabu hiyo kutamba kwa sasa wakijivunia rekodi hiyo.
Hata hivyo Yanga sc inabidi wajipange wanapokwenda kuwavaa Kmc ambao kwa sasa wamekua na moto katika ligi huku wakizitoa jasho timu kubwa ambapo walitoa suluhu na Simba sc na kuwafunga Azam Fc kwa mabao 2-1 hali iliyosababisha kocha Dennis Lavigne kutimuliwa kikosini humo siku chache zilizopita.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited