Home Makala Ngoma Kupoteza Nafasi Azam Fc

Ngoma Kupoteza Nafasi Azam Fc

by Sports Leo
0 comments

Azam FC imemuongezea mkataba mshambuliaji , Obrey Chirwa huku uongozi wa timu hiyo umeonekana hauna mpango wa kumuongezea mkataba nyota wake, Donald Ngoma.

Uongozi wa Azam FC Unadai kuwa Ngoma amekuwa hana mwendelezo mzuri ndani ya klabu hiyo kutokana na kuandamwa na majeraha ya mara kwa mara hali inayofanya ashindwe kuonyesha kiwango bora na kutoa mchango wake kwenye timu hiyo.

Ngoma alitakiwa arejee Dar kuja kuongeza mkataba pamoja na Chirwa, lakini viongozi wameona bora amalize mkataba wake aondoke na wao watafute mshambuliaji mwingine atakaye chukua nafasi yake

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited