Home Makala Okrah Arejea Benchem United

Okrah Arejea Benchem United

by Dennis Msotwa
0 comments

Aliyekuwa kiungo mshambuliaji wa klabu ya Simba sc Agustine Okrah amejiunga na klabu ya Bechem United ya Ghana baada ya kuachana na klabu hiyo kwa makubaliano ya pande zote mbili baada ya kutumika kwa msimu mmoja pekee

Kwa mujibu wa taarifa kutoka katika Moja ya jarida kubwa la Michezo la nchini Ghana jarida hilo limeripoti kuwa kiungo huyo ameingia makubaliano ya kusaini mkataba wa mwaka mmoja tu na waliokuwa Waajiri wake hao,

Mara baada ya kutambulishwa Kwa mashabiki nyota huyo amekabidhiwa jezi namba 10 alivyokuwa akiivaa kabla hajasajiliwa Simba sc.

banner

” Okrah rasmi amerejea katika klabu yake ya zamani ya Bechem aliyokuwa anaichezea kabla ya kujiunga na Simba katika msimu uliopita”,

Okrah alikua mchezaji muhimu klabuni hapo kabla hajajiunga na Simba sc ambapo majeraha yalikua kikwazo kwake kutimiza malengo yake.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited