Home Makala Pogba Kuondoka Man Utd

Pogba Kuondoka Man Utd

by Sports Leo
0 comments

Kiungo Paul Pogba imethibitika ataondoka katika klabu ya Manchester United mwishoni mwa msimu huu baada ya mkataba wake kumalizika ambapo inatajwa kuwa tayari yuko kwenye mazungumzo ya kujiunga na Juventus ama Paris st.Germans ya nchini Ufaransa.

Pogba alijiunga na Man utd akitokea Juventus mwaka 2016 miaka minne tangu aondoke Man utd kama mchezaji huru huku akirudi klabuni hapo kwa dau la rekodi ya usajili ya Paundi milioni 89 na sasa ataondoka tena kwa mara ya pili akiwa huru huku tayari Man utd imeanza mazungumzo ya awali kumsajili Frankie De Jong wa Barcelona kuchukua nafasi hiyo.

”Klabu inatangaza kwamba Paul Pogba ataondoka klabuni ifikapo mwezi juni ikiwa ni mwisho wa mkataba wake,kila mtu klabuni hapa anamshukuru Paul kwa mafanikio yake kwa Manchester United”.

banner

Mshindi huyo wa kombe la dunia akiwa na timu ya Taifa ya Ufaransa mwaka 2018 anaondoka United ambako amekaa kwa miaka sita huku akishindwa kupata mafanikio makubwa kiwanjani na inatarajiwa anaweza kurudi Juventus ama kujiunga na Real Madrid na Psg japo kwa sasa yupo mapumziko Miami Marekani na anatarajiwa kufanya maamuzi hivi karibuni.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited