Home Makala Saido Alamba Pesa nene Simba sc

Saido Alamba Pesa nene Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Staa wa zamani wa klabu ya Yanga sc Saido Ntibanzokiza amelamba dili la mkataba mnono wa kujiunga na klabu ya Simba sc kwa mkataba wa mwaka mmoja na nusu ambapo mkataba huo amelamba pesa nono kutoka kwa matajiri hao wa kariakoo.

Katika mkataba huo staa huyo amelamba pesa ya usajili kiasi cha zaidi ya milioni 60 za kitanzania pamoja na mshahara wa dola za kigeni elfu nne ambao ni zaidi ya milioni tisa za kitanzania huku pia akipewa nyumba maeneo ya masaki ama Oysterbay na mikocheni kulingana na eneo itakapopatikana kwa urahisi zaidi.

Licha ya kutambulishwa staa huyo pamoja na kuhudhuria mazoezi bado hajacheza mchezo wowote mpaka sasa huku pia akiwekewa masharti mazito kuhusu masuala ya nidhamu ikiwemo kukatwa pesa endapo atafanya utovu wowote wa nidhamu baada ya taarifa za Yanga sc kuwa alikua msumbufu mara kadhaa.

banner

Staa huyo kutoka Burundi alijiunga na Geita Gold sc akitokea Yanga  sc ambapo mpaka sasa anajiunga na Simba sc alikua amefanikiwa kutoa assisti sita na kufunga mabao matatu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited