Washambuliaji wawili wa klabu ya Yanga sc Saido Ntibanzokiza pamoja na Yacouba Sogne waliokua na majeraha waliyoyapata katika michuano ya mapinduzi Cuo visiwani Zanzibar Bado kidogo tu warudi katika hali yao ya kawaida baada ya kupona majeraha.
Awali wachezaji hao walikua wakisumbuliwa na majeraha mbalimbali lakini kwa mujibu wa kocha Cedrick Kaze tayari wachezaji hao wameanza mazoezi kurejea katika utimamu kamili wa mwili.
Wachezaji hao wamekua na mchango mkubwa kwa timu hiyo hasa katika mechi za ligi kuu nchini hivyo kurejea kwa ni faraja kwa klabu hiyo iliyoanza rasmi mazoezi kujiandaa na awamu ya pili ya ligi kuu nchini inayotarajiwa kuanza Februari 13.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.