Home Makala Samatta Aweka Rekodi Uefa

Samatta Aweka Rekodi Uefa

by Sports Leo
0 comments

Mtanzania Mbwana Samatta ameweka rekodi ya kuwa Mtanzania wa kwanza kucheza michuano ya klabu bingwa barani ulaya wakati akiichezea timu yake ya KRC Genk dhidi ya Reddbull Salzburg ya nchini Australia.

Katika mchezo huo licha ya Genk kupoteza kwa mabao 5-2 nahodha huyo aliweka rekodi nyingine ya kuwa mtanzania wa kwanza kufunga goli katika michuano hiyo baada ya kufunga kwa kicha cha kuchumpa akimalizia krosi iliyochongwa kutokea winga ya kushoto.

Licha ya kupoteza mchezo huo kwa idadi kubwa ya magoli Genk walionekana kutoa ushindani japo ugeni katika michuano hiyo mikubwa barani ulaya ulikua kikwazo cha kufanya vizuri na sasa wanajipanga kwa mchezo ujao dhidi ya Napoli ya italia.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited