Home Makala Simba sc Vs Asec Buku Tatu Tu!

Simba sc Vs Asec Buku Tatu Tu!

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imeshusha viingilio vya eneo la mzunguko katika mchezo wa kombe la shirikisho hatua ya makundi dhidi ya Asec Mimosa kutoka shilingi elfu tano mpaka elfu tatu tu.

Hayo yamesemwa na tajiri wa klabu hiyo bilionea Mohamed Dewji ili kuongeza chachu ya mashabiki kujaa uwanjani zaidi kuishangilia klabu hiyo inapokwenda kuanza safari ya kuwania kuchukua taji hilo ambalo miaka ya themanini walifanikiwa kuingia fainali lakini wakapoteza mchezo huo.

Simba sc itakua na kibarua kizito ikicheza takribani michezo mitatu ya hatuan ya makundi ndani ya siku 14 huku iktakiwa kusafiri ugenini mara moja kuwavaa USGN ya nchini Algeria.

banner

Simba sc imeingia katika hatua ya makundi ya kombe la shirikisho baada ya kuitoa Red Arrows ya nchini Zambia katika hatua ya mtoano.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited