Home Makala Simba Sc Waigomea Kaizer Chiefs

Simba Sc Waigomea Kaizer Chiefs

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imewasiliana na klabu ya Kaizer Chiefs kuwa haitafanya biashara ya kumuuza winga wao Kibu Denis Prosper ambae anahitajika na klabu hiyo chini ya kocha Nasredine Nabi.

Katika taarifa hiyo klabu hiyo imeeleza kuwa hawana nia ya kumuachia mchezaji huyo kujiunga na Kaizer Chiefs kwakuwa bado wana malengo nae kuelekea msimu ujao ambapo wanaamini jasho la mchezaji huyo linahitaji sana msimu ujao katika mapambano yote watakayoshiriki.

Taarifa za kuaminika ni kuwa Simba SC kupitia viongozi wake hawana nia ya kumuachia Kibu Denis katika dirisha lijalo la uhamisho.

banner

Hata hivyo pamoja na kocha Nasredine Nabi kujiridhisha kuhusu mchango mkubwa wa Kibu Dennis baada ya kumuona katika michezo kadhaa aliyokuwapa hapa nchini sasa inampasa kutafuta mchezaji mwingine kutokana na msimamo huo wa mabosi wa Simba Sc.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited