Home Makala Simba Sc Yahamia Kwa Sowah

Simba Sc Yahamia Kwa Sowah

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Simba Sc sasa imehamia kwa Jonathan Sowah ikitaka kumsajili baada ya kupata ofa kadhaa za kumuuza Lionel Ateba anayehitajika nchi za kaskazini mwa bara la Afrika.

Awali Sowah alihitajika na Yanga sc lakini mabosi wa klabu hiyo ni kama wamerudi nyuma kumalizia dili hilo wakihofia kuhusu nidhamu ya mshambuliaji huyo mkali wa kufunga mabao ligi kuu ya Nbc nchini.

Mabosi wa Simba Sc wamefungua mazungumzo na Singida Black Stars kuhusu kumsajili mshambuliaji huyo na kama wakifanikiwa basi watamuuza Lionel Ateba kutokana na ofa nono waliyokuwa nayo.

banner

Sowah ni aina ya mshambuliaji mwenye nguvu akiwa na kiwango kikubwa cha kufunga mabao ambapo ameonyesha hilo tangu ajiunge ligi kuu katikati ya msimu huu ulioisha lakini alifanikiwa kuwa katika orodha ya vinara wa mabao nchini.

Tayari makubaliano binafsi baina ya Sowah na Simba sc yamefanyika na kukamilika huku kikwazo kikubwa kikibaki kwa mabosi wa Singida Black Stars kukamilisha mazungumzo hayo na Simba sc kuhusu dau la kuvunjia mkataba wake klabuni hapo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited