Home Makala Simba Sc Yapambana Kupunguza Uchovu Mastaa

Simba Sc Yapambana Kupunguza Uchovu Mastaa

by Sports Leo
0 comments

Uongozi wa klabu ya Simba Sc unafanya mawasiliano ya karibu  na shirikisho la mpira nchini (TFF) ikiwezekana wachezaji wao walioko katika majukumu ya timu ya Tanzania  (Taifa Stars) baada ya mchezo dhidi ya Morocco waelekee moja kwa moja nchini Misri .

Mabosi wa Simba Sc  wanataka kupunguza urefu wa safari na kupunguza uchovu kwa wachezaji hao kuelekea mchezo wa robo fainali dhidi ya Al Masry utakaofanyika nchini Misri Aprili 2 2025.

banner

Simba wanaona safari itakuwa ndefu sana kwa wachezaji hao kama watarudi nchini Tanzania halafu waanze safari ya kuelekea Misri kwa ajili ya mchezo huo.

Mastaa wa klabu hiyo walioko nchini Morocco na Taifa Stars ni Ally Salim , Kibu Denis Shomari Kapombe , Abdulrazack Hamza , Kagoma Yusuph na Mohammed Hussein.

Mchezo utafanyika nchini humo April 2 mwaka huu katika uwanja wa New Suez  na kisha marudiano kufanyika jijini Dar es Salaam April 9 2025.

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited