Home Makala Simba Sc Yatakata Moshi

Simba Sc Yatakata Moshi

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imefanikiwa kuibuka alama tatu katika mchezo wa ligi kuu nchini dhidi ya Polisi Tanzania baada ya kuifunga mabao 3-1 katika mchezo uliofanyika katika uwanja wa Ushirika mkoani Kilimanjaro.

Simba sc ikianza na safu ya ushambuliaji chini ya John Bocco na Moses Phiri ilifanikiwa kupata mabao hayo matatu yakifungwa na Bocco dakika ya 32 ya mchezo kisha Moses Phiri alifunga mabao mawili katika dakika za 43 na 53 na kufanikiwa kuumaliza mchezo mapema.

Polisi Tanzania walipata bao la kufutia machozi dakika za nyongeza na kufanya dakika 90 kumalizika kwa ushindi wa 3-1 kwa Simba sc na kupunguza presha za mashabiki wa klabu hiyo hasa baada ya kupata sare katika mchezo dhidi ya Mbeya City Fc.

banner

Simba sc sasa imefikisha alama 31 katika michezo 14 ya ligi kuu huku ikiwa katika nafasi ya tatu ya msimamo wa ligi kuu nchini huku Yanga sc ikiongoza msimamo wa ligi kwa alama 32.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited