Home Makala Simba sc Yawasili Ruangwa

Simba sc Yawasili Ruangwa

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imewasili salama mkoani Mtwara katika wilaya ya Ruangwa kwa ajili ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya Namungo Fc utakaofanyika katika uwanja wa Majaliwa uliopo wilayani humo siku ya kesho Jumatano jioni.

Simba sc iliwasili kwa basi wilayani humo ikiwa na kumbukumbu ya kutolewa katika michuano ya kimataifa kwa penati na Wydad Casablanca wikiendi iliyopita na sasa imeelekeza nguvu zake kuhakikisha inalinda heshima kwa kutwaa taji la ligi kuu linalomilikiwa na Yanga sc.

Simba sc na Namungo ni klabu zilizo na uwezo wa kupambana huku kila klabu inaweza kupata matokeo ya ushindi dhidi ya mwenzake kutokana na kuwa na wachezaji bora na imara kwa kila upande huku nguvu ya pesa ikiwepo.

banner

Mpaka sasa katika msimamo wa ligi kuu nchini Simba sc ipo katika nafasi ya pili ikiwa na alama 63 huku Namungo ikiwa nafasi ya sita na alama 35 huku timu zote zikiwa zimecheza jumla ya michezo 26.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited