Home Makala Simba sc Yawatema Kagere,Mugalu

Simba sc Yawatema Kagere,Mugalu

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imewatema mastaa wake watatu wakiwemo  washambuliaji Meddie Kagere na Chris Mugalu pamoja na kiungo Thaddeo Lwanga baada ya kukubaliana kuvunja mikataba ya mwaka mmoja iliyobaki.

Wachezaji hao walijiunga na kambi ya mazoezi ya klabu hiyo nchini Misri lakini walirejea mapema kabla ya wengine kuja kufanya makubaliano ya kuvunja mikataba baada ya kocha Zoran Maki kutoridhishwa na viwango vyao ambapo awali aliomba muda ili awaangalie vizuri.

Mugalu na Kagere hawakuwa na msimu mzuri uliopita baada ya kushindwa kufurukuta na kuifanya Simba sc imalize ligi bila taji lolote la maana baada ya kunyakua mataji mfululizo kwa kipindi cha miaka minne.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited