Home Makala Singida Black Stars Yamtangaza Ouma Kocha Mkuu

Singida Black Stars Yamtangaza Ouma Kocha Mkuu

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Singida Black Stars imetangaza kuwa sasa itakuwa chini ya kocha David Ouma kama Kocha mkuu na  Muhibu Kanu kama kocha msaidizi wa klabu hiyo wakichukua nafasi ya Miloud Hamdi.

Hii inakuja baada ya aliyekuwa kocha wao mkuu Miloud Hamdi kutimkia kunako klabu ya Yanga kuchukua nafasi ya kocha Sead Ramovic ambaye ameachana na wanajangwani hao.

David Ouma aliwahi kuwa kocha wa Coastal Union kabla ya kutemana nao ambapo sasa atakua na jukumu hilo zito la kuhakikisha klabu hiyo inafanya vizuri katika ligi kuu nchini.

banner

Mpaka sasa katika msimamo wa ligi kuu Singida Black Stars ipo nafasi ya nne ya msimamo wa ligi kuu na inatarajiwa kuwa na mchezo dhidi ya timu ya Kagera Sugar Fc katika uwanja wa Liti mjini Singida.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited