Home Makala Singida Black Stars Yavunja Kambi Arusha

Singida Black Stars Yavunja Kambi Arusha

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya soka ya Singida Black Stars imevunja rasmi kambi yake ya mafunzo iliyofanyika kwa wiki tatu jijini Arusha iliyokua na lengo la kuingiza mbinu mpya za mafunzo kwa mastaa hao.

Mabosi wa klabu hiyo waliamua kuweka kambi hiyo maalumu baada ya ligi kuu ya Nbc nchini kusimama kwa takribani mwezi mmoja ili kupisha michuano ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (Chan) ambayo ilipangwa kufanyika hapa nchini kabla ya kughairishwa.

banner

Pia kambi hiyo ililenga kuingiza mbinu za mwalimu mpya Hamdi Miloud ambaye amejiunga na timu hiyo siku za karibuni baada ya kutimuliwa kocha Patrick Aussems.

Katika kambi hiyo timu hiyo ilicheza michezo miwili ya kirafiki dhidi ya Mbuni Fc waliyoshinda 4-0 na dhidi ya TMA waliyoshinda 2-1.

Kambi hiyo itarejea mjini Singida ili kuwakaribisha Kagera Sugar Fc katika mchezo wa ligi kuu ya Nbc Februari 7 kisha kusafiri mpaka jijini Dar es Salaam kuwavaa Kmc Februari 10.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited