Home Makala Southampton Waitibulia Man Utd

Southampton Waitibulia Man Utd

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Southampton imeharibu ndoto ya mashabiki wengi wa Manchester United ya kumaliza katika nafasi ya nne baada ya kusawazisha bao dakika za lala salama na kufanya matokeo ya mechi hiyo kuwa sare ya 2-2.

Southampton walikua wa kwanza kupata bao kupitia kwa Stuart Armstrong dakika ya 12 kisha Marcus Rashford akasawazisha dakika ya 20 na baadae Bruno Fernandes kumpa pasi ya mwisho Anthony Martial aliyefunga bao la pili dakika ya 23.

Wakati Mashabiki ya Man United wakitarajia mchezo kumalizika kwa matokeo hayo Michael Obafemi alisawazisha na kufanya mechi kumalizika 2-2 hivyo kuifanya Man United isalie nafasi ya tano ya msimamo kwa tofauti ya pointi moja na Chelsea mwenye pointi 60.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited