Home Soka Stars Yafuzu Chan 2025

Stars Yafuzu Chan 2025

by Sports Leo
0 comments

Timu ya Taifa ya Tanzania kwa wachezaji wa ndani imefanikiwa kufuzu michuano ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani itkayofanyika nchini mwaka 2025.

Kikosi cha timu hiyo kimefuzu licha ya kupoteza mchezo huo wa marudiano uliofanyika katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam baada ya kumaliza dakika 90 za mchezo huo kwa kushinda bao 1-0 likifungwa na Crispin Ngushi dakika ya 34 na kufanya matokeo ya jumla kuwa 1-1 na mchezo kwenda kwenye hatua ya matuta ambapo Stars ilipoteza mchezo huo kwa penati 5-6 za Sudan.

Kutokana na Tanzania kuwa mwenyeji wa michuano hiyo,imefuzu kushiriki michuano hiyo pamoja na kufungwa na Sudan.

banner

Michuano hiyo itakayofanyika kwa mara ya kwanza nchini Tanzania ambapo pia ikitumika kama njia ya kufanya tathmini kuona kama nchi itakua tayari kwa ajili ya maandalizi ya michuano ya mataifa ya Afrika mwaka 2027 ambayo utafanyika kwa Ushirikiano wa Tanzania,Kenya na Uganda.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited