Home Makala Timu 12 Kusaka Pointi 3 Leo

Timu 12 Kusaka Pointi 3 Leo

by Sports Leo
0 comments

Msimu mpya wa ligi kuu Tanzania bara unaoanza leo Septemba 6 unakutanisha timu 12 kuvaana katika viwanja tofauti ili kusaka pointi tatu muhimu kwani zote zinahitaji kutwaa taji la ligi kuu bara.

Simba Sc ambao ni mabingwa watetezi wa ligi kuu bara wapo ugenini Mbeya kumenyana na Ihefu FC katika uwanja wa Sokoine huku watani wao wa jadi, Yanga Sc watavaana na Tanzania Prisons uwanja wa Mkapa.

Namungo Fc itawakaribisha Coastal Union uwanja wa Majaliwa huku Biashara United ikimalizana  na Gwambina Fc uwanja wa Karume.

banner

Dodoma Jiji itamenyana na Mwadui Fc Uwanja wa Jamhuri ,Dodoma huku Mtibwa Sugar wakigalagazana na Ruvu Shooting huko Morogoro uwanja wa Gairo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited