Home Makala Tuzo Ya Mchezaji Bora 2020 Yafutwa

Tuzo Ya Mchezaji Bora 2020 Yafutwa

by Sports Leo
0 comments

Shirikisho la Kimataifa la Soka (FIFA) limetangaza kufuta tuzo za soka zinazotolewa na Shirikisho hilo mwaka huu kutokana na janga la virusi vya Corona ambazo zilitarajiwa kutolewa jijini Milan nchini Italia, Septemba 2020.

Washindani wawili duniani ambao ni Lionel Messi anayekipiga Barcelona na Cristiano Ronaldo wa Juventus  hawatakuwa na cha kubeba mwaka huu Kwenye kipengele cha mchezaji bora wa mwaka.

Gianni Infantino, ambaye ni Rais wa FIFA amekuwa akiweka wazi msimamo wake kuwa wanachukua tahadhari kubwa dhidi ya janga la virusi vya Corona na kuhusu tuzo za Ballon d’Or ambazo zimekuwa zikitolewa kila mwaka tangu 1956 haijulikani hatma yake mpaka sasa.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited