Home Makala Wa Kawaida Kabisa

Wa Kawaida Kabisa

by Sports Leo
0 comments

Afisa habari wa klabu ya Yanga sc Ally Kamwe amesema kuwa klabu hiyo haiwahofii wapinzania wao katika raundi ya pili ya michuano ya klabu bingwa barani Afrika ambao ni klabu ya Al Hilal Fc ya nchini Sudan licha ya kuwa wapinzani hao wana kikosi cha gharama zaidi.

Kamwe alisema hayo wakati akifanya mahojiano na kituo cha habari cha Wasafi Fm ambapo alisisitiza kuwa Yanga sc wana kikosi bora na chenye muungano kushinda Wasudan hao kwa maana wanategemea zaidi uwezo wa mchezaji mmoja mmoja.

“Yanga ni Timu bora Tanzania, kwa Squad ambayo tuko nayo, Squad ambayo imekwenda unbeaten michezo 41 ya Ligi,Hii rekodi angekuwa nayo Al Hilal, Yanga tusingelala, lakini watu hawawaambii Al Hilal kama wanakuja kucheza na Dubwasha ambalo limecheza michezo 41 bila kufungwa, na hiyo michezo 41 wapambe wenu wapo,”Alisema Kamwe

banner

Mbali na mchezo huo pia aligusia namna klabu hiyo ilivyofanya mchakato wa mabadiliko halisi kuelekea katika mfumo mpya wa uendeshaji wa klabu hapa nchini “Nilikuwa nasikia tu kuhusu mabadiliko lakini nimekuja kuyaona Yanga, hakuna Timu ikiyofanya Mabadiliko Sahihi ya Mpira kuliko Yanga Sc, Injinia amelipa Pesa nyingi sana La liga kupata huo ushauri wa kiendeshaji”

Yanga sc itacheza na Al Hilal ya kocha Florent Ibenge katika mchezo wa kwanza ambao utafanyika hapa nchini siku ya Jumamosi Oktoba 8 na marudiano yatafanyika nchini Sudan siku ya Oktoba 16.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited