Home Makala Walibya Watua kwa Fabrice Ngoma

Walibya Watua kwa Fabrice Ngoma

by Sports Leo
0 comments

Kiungo wa klabu ya  Simba Sc Fabrice Ngoma amefikia makubaliano binafsi ya kujiunga na klabu ya Al-Ittihad Tripoli ya Libya.

Tayari staa huyo amepokea ofa nono ya Mshahara na dau la usajili  (Sign-on fee) kutoka Al-Ittihad na tayari amesema ndio ambapo sasa imebaki kwa Simba sc kukubali uhamisho huo.

Kilichobaki ni makubaliano kati ya Simba Sc na Al-Ittihad na kuanzia muda wowote  sasa klabu hiyo tajiri ya Libya itatuma ofa Msimbazi kuhusu dau la kununua mkataba wa staa huyo raia wa Congo Drc.

banner

Mkataba wa Ngoma na Simba umebakiza miezi mitano hivyo kisheria anaruhusiwa kuongea na timu yeyote japo amekua akiipa nafasi zaidi Simba sc endapo itahitaji kumuongezea mkataba.

Dirisha la usajili la Libya litafungwa mwishoni mwa mwezi huu na Al-Ittihad wanamuhitaji NNgoma mapema ili kukamilisha sajili zao na kama Simba watakubaliana na ofa ya Al-Ittihad basi nyota huyo ataondoka haraka sana.

Baada ya kukamilisha usajili wa Mahmoud Kahraba kutoka Al Ahly,sasa Ittihad wamemgeukia Ngoma.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited