Home Makala Wawa Aondoka Singida Big Stars

Wawa Aondoka Singida Big Stars

by Sports Leo
0 comments

Beki wa zamani wa klabu ya Simba sc Serge Paschal Wawa ameondoka katika klabu ya Singida Big Stars baada ya kumalizana na klabu hiyo aliyojiunga nayo akitokea klabu ya Simba sc ambapo amedumu kwa takribani nusu msimu  pekee.

Wawa kwa mara ya kwanza alitambulishwa na Azam Fc nchini misimu kadhaa nyuma miaka ya 2014 ambapo alidumu Azam Fc kwa misimu miwili kabla ya kujiunga tena na El-Merrekh Fc ya nchini Sudan alipotokea kisha akajiunga na Simba sc alipokaa kwa miaka mitano mpaka msimu huu mwanzoni alipojiunga na Singida Big Stars.

Wawa ameondoka klabuni hapo baada ya kushindwa kuwa na kiwango bora ambapo mara kadhaa amesababisha timu hiyo kufungwa kutokana na kukosa umakini katika kutuliza mashambulizi ya wapinzani ambapo klabu hiyo imemsajili beki mpya kutoka Brazil Marcos Wilson da Silva kuziba nafasi hiyo ambaye atashirikiana na Biemesi Carno.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited