Home Makala Willian Anukia Anfield

Willian Anukia Anfield

by Dennis Msotwa
0 comments

Kiungo anayekipiga ndani ya klabu ya Chelsea iliyo chini ya Frank Lampard,Willian Borges da Silva, inaelezwa kuwa yupo kwenye mazungumzo na klabu ya Liverpool baada ya kuwa na mvutano kati yake na mabosi wake ambao wanataka kumpa dili la mwaka mmoja huku yeye akihitaji kupewa kandarasi ya miaka miwili.

Liverpool iliyo chini ya Jurgen Klopp tayari imeanza hesabu za kuinasa saini yake ili kandarasi yake itakapomeguka ndani ya Chelsea aibukie Anfield.

Borges da Silva mwenye umri wa miaka 31 amejiunga na Chelsea mwaka 2013 na mkataba wake unakaribia kumeguka June,30 mwaka huu pia amecheza mechi 28 kwenye msimamo wa ligi kuu kabla ya kusimama na amefunga mabao 5 na kutoa asisti 5.

banner

sea

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited