Home Makala Wydad Watua Kibabe

Wydad Watua Kibabe

by Sports Leo
0 comments

Kikosi cha klabu ya Wydad Casablanca kimewasili nchini jioni ya leo kwwa ajili ya mchezo wa siku ya Jumamosi wa hatua ya robo fainali ya ligi ya mabingwa dhidi ya Simba sc utakaofanyika saa kumi jioni katika uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar es salaam.

Msafara wa kikosi hicho umewasili na kupokelewa na maafisa wa klabu ya Simba sc sambamba na waandishi wa habari waliokua wakichukua picha na kufanya mahojiano na baadhi ya mastaa wa klabu hiyo hasa wale wanaojua kiingereza na kiswahili.

Wydad AC wametua  leo  wakiwa na msafara wa watu 50 na wamekuja na ndege ya kukodi moja kwa moja kutoka nchini Morroco mpaka hapa nchini huku baadhi ya mabosi wa klabu hiyo wakiwa wameshawasili tangu siku ya Jumamosi kwa ajili ya kuweka mazingira sawa.

banner

Baada ya mchezo huo Simba sc italazimika kusafiri kwenda nchini Morocco kwa ajili ya mchezo wa marudiano ukaofanyika Jumamosi ya April 30 mwaka huu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited