Timu ya soka ya Yanga sc imetolewa kwenye michuano ya kombe la mapinduzi baada ya kufungwa kwa mikwaju ya penati na Mtibwa Sugar baada ya kutoka sare ya bao 1-1 ndani ya dakika 90.
Mtibwa walipata penati 4 huku yanga wakifunga 2 huku Kelvin Yondani na Abdulaaziz Makame wakikosa kwa upande wa Yanga na Abdulhalim Humoud akikosa kwa upande wa Mtibwa Sugar.
Waliofunga kwa upande wa Yanga ni Paulo Godfrey,Balama Mapinduzi huku Jafary Kibaya,Kibwana Shomari na Dickon Job wakipata mikwaju yao.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Mtibwa walisawazisha goli la dakika ya 37 la Deus Kaseke kupitia kwa Kibwana Shomary dakika ya 90+3 na kuelekea Hatua ya matuta ambapo baada ya kuibuka na ushindi watasubiri mshindi kati ya Simba sc dhidi ya Azam fc ili kucheza fainali.