Home Soka Yanga Sc Yaibamiza Prisons Fc

Yanga Sc Yaibamiza Prisons Fc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga sc imefanikiwa kuchukua alama tatu katika mchezo wa ligi kuu ya Nbc nchini dhidi ya Klabu ya Tanzania Prisons uliofanyika katika uwanja wa Kmc Complex uliopo Mwenge jijini Dar es Salaam.

Katika mchezo huo ilishuhudiwa dakika tisini zikikamilika kwa Yanga sc kupata ushindi wa mabao 4-0 huku Ibrahim Bacca akiwa mchezaji bora wa mechi baada ya kufunga mabao mawili kati ya manne.

Clement Mzize alifungua kalamu ya mabao baada ya kupata pasi nzuri ya Prince Dube dakika ya 13 kisha Bacca aliunganisha mpira uliogonga mwamba wa Aziz Ki dakika ya 42 ya mchezo huo huku dakika tatu baadae Dube alifunga bao la tatu akipokea pasi ya Stephan Aziz Ki.

banner

Baada ya Mapumziko Prisons iliamua kurudi nyuma na kuzuia ili isifungwe mabao mengi lakini walijisahau dakika ya 83 ya mchezo na kuruhusu bao la kichwa la Ibrahim Hamad Bacca na kufanya mchezo huo kumalizika kwa Yanga sc kupata mabao 4-0.

Kocha Sead Ramovic baada ya mchezo huo alisema kuwa ushindi huo umetokana na wachezaji wake kujituma dakika zote.

“Tulikuwa na mechi ngumu wote,nawapongeza wapinzani kwa mechi ngumu,tumeongeza fitness yetu na nyie wote mnaona sasa, najivunia kuwa kocha wa hii timu na kuongoza kundi hili la wachezaji na inshallah mwishoni tutakuwa na wakati nzuri.” Alisema Ramovic

Yanga sc sasa imefikisha alama 33 ikiwa nyuma ya Simba sc kwa alama moja baada ya kucheza michezo 13 ya ligi kuu ya Nbc nchini.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited