Home Makala Yanga sc Yaifunga Asas Fc

Yanga sc Yaifunga Asas Fc

by Sports Leo
0 comments

Mabao mawili ya Aziz Ki na Kennedy Musonda yameiwezesha klabu ya Yanga sc kuibuka na alama tatu katika mchezo wa awali wa michuano ya klabu bingwa barani Afrika dhidi ya Asas Fc ya Djibout.

Mchezo uliofanyika katika uwanja wa Chamazi Complex jijini Dar es salaam ambapo Yanga sc ilikua mgeni ilifanikiwa kutawala dakika zote tisini za mchezo japo ufanisi mdogo katika safu ya ushambuliaji uliwafanya kumaliza mchezo ikiwa na mabao hayo mawili pekee.

Safu ya ushambuliaji chini ya Kennedy Musonda na Clement Mzize mpaka sasa bado inashindwa kumalizia nafasi nyingi wanazopata Yanga sc licha ya kupewa mipira lukuki na safu ya kiungo ya klabu hiyo.

banner

Mchezo wa marudiano unatarajiwa kufanyika Augusti 26 ambapo Yanga sc itakua mwenyeji na utafanyika katika uwanja huo huo ambapo mshindi wa jumla michezo hiyo miwili atafuzu hatua ya pili ambapo watakutana na mshindi kati ya Al-Merreck na Otoho d’oyo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited