Home Makala Yanga sc Yaimaliza Kmc

Yanga sc Yaimaliza Kmc

by Sports Leo
0 comments

Ikianza na kikosi cha wachezaji wengi ambao wanaanzia benchi Yanga sc imefanikiwa kupata alama tatu katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Kmc uliofanyika katika uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar es salaam.

Yanga sc ilipata bao hilo dakika ya 38 kupitia kwa Clement Mzize aliyeunganisha mpira uliotemwa na kipa David Kissu Mapigano aliyeshindwa kuokoa mpira wa kona na kumkuta mfungaji huyo kinda aliyeanza badala ya Fiston Mayele.

Mzize aliyesaidia na Stephane Aziz Ki sambamba na Dickson Ambundo na Tuisila Kisinda alikosa mabao kadhaa ya wazi kutokana na kukosa utulivu katika eneo hilo la mbele.

banner

Kmc licha ya kujitahidi kusawazisha bao hilo milango ilikua migumu upande wao kutokana na uwezo wa kipa Djigui Diarra katika kuwapanga mabeki wake wakiongozwa na nahodha Bakari Mwamnyeto aliyecheza pacha na Ibrahim Abdalah Bacca.

Yanga sc sasa imefikisha alama 62 katika michezo 23 ya ligi kuu ikiiwaacha Simba sc kwa alama nane huku zikiwa zimesalia mechi saba kwa kila timu kumaliza msimu wa ligi kuu nchini.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited